Wednesday, June 26, 2019

Mshauri Mkuu wa AZCA apeleka zawadi kwa mgonjwa.

Kushoto ni Mshauri mkuu wa Jumuiya ya kusaidia watoto Zanzibar (AZCA) Hidaya Ali Muhamed akimkabidhi Bi Fadhila Malik Juma zawadi ya Pempas zilizotolewa na taasisi hii.

Tukio hili ni la jana 25 june 2019 huko ZIWATUWE  Amani Zanzibar baada ya jumuiya kumsafirisha mama huyu ambae mwanawe anasumbuliwa na kutopata choo tokea kuzaliwa kuja kisiwani Unguja kwaajili ya Matibabu.

Mtoto huyo anaesumbuliwa na ugonjwa huo anaumri wa mwaka mmoja na miezi 5 na alianza tukio hilo tokea siku alipozaliwa na taasisi yako Pendwa jana ilimtembelea kwa lengo la kumfariji pamoja na kufanya nae mazungumzo juu ya kinachotakiwa katika matibabu ya mtoto.

No comments:

Post a Comment