
Tukio hili ni la jana 25 june 2019 huko ZIWATUWE Amani Zanzibar baada ya jumuiya kumsafirisha mama huyu ambae mwanawe anasumbuliwa na kutopata choo tokea kuzaliwa kuja kisiwani Unguja kwaajili ya Matibabu.
Mtoto huyo anaesumbuliwa na ugonjwa huo anaumri wa mwaka mmoja na miezi 5 na alianza tukio hilo tokea siku alipozaliwa na taasisi yako Pendwa jana ilimtembelea kwa lengo la kumfariji pamoja na kufanya nae mazungumzo juu ya kinachotakiwa katika matibabu ya mtoto.
No comments:
Post a Comment