Thursday, July 18, 2019

CHANGIA KUTENGENEZA AGHERA YAKO, WATOTO WAOZA MACHO NA USO


Assalam Alykum Warahmatullahi Wabarakatuh?

Hawa ni watoto kutoka kijiji cha Junguni, Wete Kisiwani Pemba nchni Tanzania (Zanzibar) ambao ni Husna na Riziki Hamadi , mmoja wa miaka 19 na mwengine miaka 6.

Siku chache zilozopita walipatwa na homa, badae wakaanza kuoza  macho kisha uso na mwili wote, wazazi wameshafuatilia matibabu katika hospitali tofauti lakini imeshindikana hasa kwakua hawana pesa za kujikimu katika matibatu.

Hali za familia ya watoto hawa kiuchumi ni mbaya sana, tunakuomba msaada wako kuchangia fedha kwa lengo la kuwapatia matibabu hata ikiwezekana nje ya nchi, tatizo kubwa ni hali mbaya kifedha na kama una uwezo wa kuwafanyia mpango matibabu wewe pia unakaribishwa.

Taasisi yako ya AZCA inabeba jukumu la kukuomba msaada kwa watoto hawa baadae kuwashuhulikia matibabu ili waendelee kuishi kwa Amani, kwani bado wanahitaji kusoma na kuishi vizuri, changia kwaajili ya ALLAH SUBHAANAHU WATAALA, SADAKA YAKO UTAIKUTA MBELE YA MUNGU.

Mawasiliano +255774181532 / +255774253759

Nambari ya kuchangia pesa (tigo pesa) +255672560173

No comments:

Post a Comment