Assalam
Alykum Warahmatullahi Wabarakatuh ?
Awali ya yote tuna mshukuru Muumba kutupa nguvu ya
kulisimamia hili.
Watoto wetu tuliwafikisha katika Hospitali Kuu ya Mnazi mmoja
Unguja kwa matibabu na Alhamdulillahi walifanyiwa huduma kadiri ilivyowezekana
hapo.
Siku mbili nyuma, yaani juzi baada ya hatua kukamilika
tulifanikiwa kuwasafirisha wote watatu pamoja na wazee wao hadi katika
hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam ambapo hadi hivi sasa wanaendelea
kupokea matibabu na hali zao zinaendelea vizuri.
Tunakujuza taarifa hii ili tu ujue kinachoendelea na taarifa
rasmi itafutia baada ya hatua zote kukamilika.
Watoto hao wapo chini ya usimamizi wa taasisi ya ALL FOR
ZANZIBAR CHILDREN ASSOCIATION – AZCA na inahakikisha wanapata huduma nzuri za
matibabu.
Taasisi inawashukuru wale wate waliyojitokeza kutoa michango
yao ya hali na mali kufanikisha kupatiwa matibabu haya, ahsanteni na hongereni
sana, lakini pia musituache mkono kwani safari hii ya matibabu ni ndefu sana.
Baadae tutatoa tena taarifa nini kinatakikana.
Ahsanteni
Imetolewa na
Afisa habari na
uhusiano
All for Zanzibar
children association – AZCA