Monday, August 12, 2019

PINGA UDHALILISHAJI , NI ADUI WA HAKI ZA WATOTO.

Mara nyingi unaposikiliza vyombo vya habari hukosi kusikia tukio la udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto nchini Zanzibar, tatizo hili linaonekana kuwa kubwa kiasi, hivyo taasisi ya AZCA  imeamua kubuni kila njia kuhakikisha inasaidia kuondosha tatizo hili ambalo wahanga wakubwa ni watoto na mamazao.



Ingawa juhudi hizo zimenza katika nyanja tofauti kama vile kupita madrasa kutoa taaluma ya kujiweka mbali na udhalilishaji nk. pia taasisi imepata nafasi ya kushirikia katika kituo cha radio swahiba fm na kutoa taaluma hiyo kwa jamii.


Ni imani yetu wanajamii walitusikia vyema na matumaini yetu kila mmoja awe mwalimu kwa mwenzake kumuhamasisha kupiga vita matukio haya mabaya ya udhalilishaji yanawakosesha haki  za msingi watoto kama vile haki ya elimu na kutembea.


No comments:

Post a Comment