Inafahamika
kuwa kipindi cha Skukuu kila mmoja anatakiwa awe na furaha ili mambo
yaende sawa, chakusikitisha kuna makundi ya watu katika jamii tunazoishi
wanafikiwa na skukuu wakiwa hawana furaha kabisa, likiwamo kundi la Watoto
yatima.
Kiuhalisia,
uyatima unauma, lakini unazidi kuuma sana
katika masiku kama haya, mtoto anawaza siku ya leo angaekuwepo baba angekua ameshapata
nguo, "angekuwepo baba ningepata pesa" hasa akiwaona wenzake
wamependeza na kwenda viwanjani.
Shukran
za dhati zimfikie aliyejitokeza kuchangia kutoa vitambaa vya kushonewa nguo
watoto wayima ili wajihisi kuwa si watofauti na wawe na furaha, tunamshukuru
mungu jukumu hili tumelisimamia vizuri na siku
mbili kabla ya skukuu tuliwapatia vitambaa hivyo watoto yatima ambao
tunawasimamia, tunakuomba nawe mwenye nguo hata za mtumba, toys za kuchezea,
pesa, nk tuletee, jicho lao ni sisi , changia ili kuwafanya wawe na furaha,
hawana pakuendea isipokua kwa waisilamu wenzao, njoo ujenge pepo yako kwa
kuwaokoa watoto yatima.
Nambari
zetu kama zinavyoonekana mtandaoni na hapa
tunakuwekea..+255774181532/+255624432662/+255777374545
ACNT
: NMB NO: 22910033046 Jina: All For
Zanzibar Children Association
No comments:
Post a Comment